#Mapinduzi #serengeti #shule
Shule ya msingi Mapinduzi iliyoko Mara wilaya ya serengeti kata ya morotonga National imeanzishwa mwaka 1977 inazochangamoto nyingi zinazoikabili pamoja na Upungufu wa ukarabati wa madarasa hali inayopelekea wanafunzi hao kusoma kwa kubadilishana asubuhi na mchana
Mkuu wa shule GODRIVA ERNEST amewaomba wadau mbali mbali wa maendeleo katika wilaya yetu ya serengeti kujumuika katika ukarabati wa madarasa ilii kuhakikisha taaluma inapanda katika shule hio
Hata hivyo GODRIVA ERNEST amesema licha ya kuwa na mkakati wa wazazi wote katika mtaa wa national kushiriki katika uchangiaji wa zoezi hilo lakini fedha hizo hazitoweza kukidhi ukarabati huo
Nae kwa upande wake Mwenyekiti wa kitongoji JONGO MATUSI amekazia juu ya kuwaomba wadau hao kuwasaidia katika ukarabati huo ikiwemo WORLD CHANGER,SENAPA,IKONA WMA,GRUMETI FUND na wengineo
Category
Show more
Comments - 5
Related videos for CHANGAMOTO YA MADARASA SHULE YA MAPINDUZI/ OMBI KWA WADAU NA SERIKALI KUWAUNGA MKONO UKARABATI HUO: